Pages

Ads 468x60px

Thursday, November 28, 2013

UGANDA YAENDELEA KUZIBURUZA NCHI WANACHAMA WA CECAFA KATIKA MSIMAMO WA UBORA WA SOKA DUNIANI




Tanzania imepanda kwenye msimamo wa ubora wa soka duniani kwatakwimu zilizotolewa leo na shirikisho la soka duniani Fifa.
Takwimu hizo ambazo hutolewa kila mwezi Tanzania ipanda kwa nafasi tano kutoka nafasi ya 129 mwezi uliopita hadi katika nafasi ya 124 mwezi huu.

Katika takwimu hizo Uganda imeendelea kushika nafasi ya kwanza  kwa nchi wanachama wa Cecafa kwakuwa nafasi ya 86 kidunia huku Ethiopia ikishika nafasi ya pili kwa ukanda huo huku kidunia ikiwa nafasi ya 93.

Burundi ya 112 kidunia kwaukanda Cecafa inashika nafasi ya tatu,Kenya ya 4 kwa ukanda huo ikiwa nafasi ya 117 kidunia huku nafasi ya 5 kwa ukanda wa Cecafa ikishikwa na Tanzania iliyopo nafasi ya 124 kidunia.
Rwanda inashika nafasi ya 6 kwa ukanda wa Cecafa ikiwa nafasi ya 127 kidunia,Sudani inashika nafasi ya 7 kwa Cecafa huku ikishika nafasi ya 130 kwa dunia.

Katika msimamo huo wa ubora wa soka duniani Eritrea inashika nafasi ya 8 kwa nchi wanachama wa Cecafa kidunia ikishika nafasi ya 199,Sudan Kusini inashika nafasi ya 9 kwa ukanda wa Cecafa wakati kidunia ikishika nafasi ya 201.

Somalia ndiyo inayoburuza mkia kwenye takwimu hizo za obora wa soka duniani kwa nchi wanachama wa Cecafa ikishika nafasi ya 10 huku kidunia ikishika nafasi ya 204.

mkule.blogspot.com

No comments:

Post a Comment