Kiungo wa klabu ya Real Madrid na timu ya
taifa ya Ujeruman Sami Khedira atakuwa nje ya uwanja kwa miezi sita kutokana na
kusumbuliwa na jeraha la goti.
Khedira mwezye umri wa mika 26 aliumia jana
katika mchezo wa kirafiki baina ya timu yake ya taifa ya Ujerumani ilipokuwa
ikicheza na Italia mjini Milan pambano liloloisha kwa sare ya kufungana goli 1
kwa 1.
Mchezaji huyo ambaye ameichezea timu ya taifa
ya Ujerumani michezo 44 sasa anasubiri kufanyiwa upasuaji kutibu jeraha hilo
Akizungumza kwa masikitiko makubwa kocha wa
Ujeruma Joachim Low amesema anatambua
mchango wa ntota huyo katika kikosi chake lakini anamatumaini kwamba atapona kabla ya fainali zijazo za
kombe la dunia zitakzofanyika mwakani nchini Brazil.
Kuumia kwa kiungo huyo si pigo kwa Ujerumani
pekee bali hata kwa klabu yake ya Real Madrid ambayo inapigania ubingwa wa ligi
kuu ya Hispania pamoja na kombe la klabu bingwa barani Ulaya msimu huu.
Posted by Yusuph Mkule.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment