Pages

Ads 468x60px

Friday, November 15, 2013

KATIBU MKUU WA RT AFUNGA KOZI YA WAKUFUNZI WA RIADHA KATIKA CHUO CHA UALIMU KLERUU MKOANI IRINGA LEO.



Kozi ya wakufunzi wa mchezo wa riadha iliyokuwa ikifanyika katika chuo cha ualimu Kleruu imemaliza leo kwakufungwa na katibu mkuu wa shirikisho la riadha nchini RT Suleiman Nyambui huku wahitimu 31 wakikabidhiwa vyeti vyao.
Kozi hiyo ambayo ilihusisha walimu mbalimbali wa shule za msingi  wa chuoni hapo na walionje ya chuo hicho ilikuwa ikihusisha mafunzo ya daraja la kwanza na la pili ambapo jumla ya wahitimu waliomaliza ni 31.
Kati ya hao waliohitimu daraja la kwanza ni 12  wanawake watano wanaume 7 huku daraja la pili wakihitimu watahiniwa 19  wanawake 8 wanaume 11.
Akizungumza katika hafla maalumu ya kukabidhi vyeti kwa wahitimu hao katibu mkuu wa Shirikisho la riadha nchini RT Suleiman Nyambui amewataka wahitimu kutumia vyema mafunzo waliyoyapata katika kuendeleza mchezo huo.
Nyambui amesema jitihada kubwa zinahitajika kurejesha heshima ya mchezo wa riadha iliyopotea  kwa muda mrefu huku akitoa rai kwa vyuo mbalimbali kutoa mafunzo ya riadha kwa wanafunzi kwa lengo la kuuendeza mchezo huo.

Amesema wao kama shirikisho wapo tayari kufika mahala popote kutoa mafunzo za ukufunzi wa mchezo wa riadha bila malipo yeyote kikubwa ni kugharamia nauli za wakufunzi chakula pamoja na malazi kwa muda ambao kozi itakuwa ikitolewa.

Aidha ameushukuru uongozi wa chuo cha ualimu Kleruu kwa kuwa mstari wa mbele kuendeleza riadha kwatoa fursa kwa walimu chuoni hapo kupata mafunzo hayo.
Naye mgeni rasmi katika hafla hiyo afisa michezo mkoa wa Iringa Kenethi Komba ameseahidi kushirikiana na chuo cha Kleruu pamoja na shirikisho la riadha nchini RT  katika harakati za kuendeleza mchezo huo mashuleni.
Amesema kushuka kwa mchezo wa riadha nchini kunatokana na serikali kuondoa michezo mashuleni kabla ya kuirejesha tena huku akiwaomba wahitimu kutumia vyema mafunzo waliyoyapata kwenye  maeneo yao ya kazi.
Kozi hiyo ilikuwa ikisimamiwa na mkufunzi mkuu anayetambuliwa na shirikisho la riadha nchini RT  ndg.Samweli Tupa ambaye alikuwa kivutio kikubwa kwa wahitimu hao  kutokana na ucheshi  alionao katika ufundishaji.





Mgeni rasmi akitoa cheti kwa mmoja wa wahitimu wa kozi hiyo mchana wa leo.




Katibu mkuu wa rt Suleiman Nyambui akizungumza na wahitimu wa kozi hiyo katika chuo cha kleruu katikati ni mgeni rasmi Keneth Komba ambaye ni afisa michezo mkoa wa iringa na wapembeni yake ni mwl.Samweli Tupa aliyekuwa mkufunzi wa kozi hiyo.




Wahitimu  katika igizo la huwezi kumtambua mwathika wa ugonjwa wa ukimwi kwa kumwangalia ambapo kila upande mtu mmoja alipatiwa kitu wakiwa wamefumba macho na kisha kuanza zoezi la kukisia ni nani anaedhaniwa kuwa mwathirika kwakuangalia mshindi ni aliyepatia mtu mwenye kitu alichopewa na mmoja wa washiriki. 


 
Mkufunzi Samweli Tupa akizungumza jambo mbele ya wahimu hao mchana wa leo .


Posted by Yusuph Mkule.

No comments:

Post a Comment