Zidan akiwa katika jezi ya timu ya taifa ya Misri.
Mshambuliaji
wa zamani wa timu ya taifa ya Misri na Klabu vya Borussia Dortmund amehukumiwa
kwenda jela miaka 6 baada ya kukutwa na kosa la kuandika cheki tatu za uongo
kwenye kampuni mmoja ya kibiashara
iliyopo Misri.
Kwamujibu wa vyombo vya habari nchini Misri
mahakama imemkuta na hatia mchezaji huyo
na kujiridhisha mtuhumiwa kutenda kosa hilo kwenye kampuni hiyo hivyo
atatumikia kifungo hicho .
Zidan mwenye umri wa miaka 31 enzi za uchezaji
wake alifanikiwa kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya Ujerumani Bundesiliga alkiwa na
Borussia Dortmund huku akishinda ubingwa wa Afrika mara mbili akiwa na timu ya
taifa ya Misri.
Hadi anakutwa na mkasa huo wa kuhukumiwa
kwenda jela miaka sita Zidan alikuwa akifanya kazi katika shirika la habari la
Aljazira mjini Doha kama mchambuzi wa michezo kwenye kituo hicho.
Hapa Zidan akiwa na uzi wa timu ya taifa ya Misri kwenye mchezo dhidi ya Brazil
Hapa Zidan akiwa na uzi wa timu ya taifa ya Misri kwenye mchezo dhidi ya Brazil
Hapa akiwa na jezi ya klabu ya Borussia Dortmund ya nchini Ujeruman.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment