Mabingwa wa
ligi kuu ya soka Tanzania bara timu ya Yanga
wamefanikiwa kumaliza duru ya kwanza
msimu huu wa 2013/2014 wakiongoza
ligi baada ya kufanikiwa kuinyuka Jkt Oljoro ya mkoani Arusha magoli
3 kwa 0 pambano lilochezwa hapo
jana kwenye dimba na taifa jijini Daresalaam.
Yanga ambayo
ilianza ligi kwa kusuasua imefanikiwa
kuvuna alama 28 katika michezo 13 waliyocheza msimu huu wakishinda michezo
minane,kwenda sare minne na kufungwa
mchezo mmoja pekee chini ya kocha mkuu Arne Brandts raia wa Uholanzi.
Kwaufupi Yanga
wameonyesha uwezo mzuri licha ya kukabiliwa na upinzani mkubwa kwenye
michezo yao ya ugenini msimu huu lakini wameendelea kuwa wakomavu kwa kuutumia vyema uwanja wao
wa nyumbani wa taifa kila wanapocheza.
Je,kasi waliyomaliza nayo wataanza nayo vijana hao wenye kibarua cha kuutetea ubingwa mbele ya Mbeya City na Azam walioonyesha upinzani mkubwa msimu huu?
Je,kasi waliyomaliza nayo wataanza nayo vijana hao wenye kibarua cha kuutetea ubingwa mbele ya Mbeya City na Azam walioonyesha upinzani mkubwa msimu huu?
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment