Kocha mkuu wa mabingwa wa ligi kuu
ya England Manchester United David Moyes amethibitisha kuwa mlinzi Nemanja Vidic atarejea uwanjani mwishoni mwa
juma hili ambapo Man U itakuwa ugenini kucheza na Cardiff City.
Matumaini ya kumrejesha uwanjani
Vidic yanatokana na kuendelea vyema kutokana na jeraha aliloumia kwenye pambano
dhidi ya Arsenal ambapo Arsenal ililala kwa kufungwa goli 1 kwa 0 lililofungwa
na Rubin Vab Persie.
Kocha David Moyes amesema jeraha
alilokuwanalo Vidic lilimlazimu apumzike kwa muda mrefu hivyo anaamini nyota
huyo raia wa Serbia ameshapumzika vyakutosha na ni wakati wake wa kurudi
uwanjai kuitumikia timu yake.
Wakati Vidic akirejea uwanujani juma
hili matumaini mengine ya United yapo kwa kiungo Michael Carrick ambaye naye
anaendelea vyema kupona na anatarajiwa kurudi dimbani siku chache zijazo.
Wakati huohuo klabu ya Manchester
United leo imerefusha mkataba wa kiungo Michael Carrick mwenye umri wa miaka 32
utakaomfanya aendelee kuwepo Old Traford hadi mwezi juni mwaka 2015.
United pia itamkosa Danny Welbeck
amabye anataraji kufanyiwa upasuaji wa goti linalomsumbua lakini pia United
kwenye mchezo wa keshokutwa huenda
ikamkosa Phil Jones ambaye aliumia akiwa akiitumiakia na timu ya taifa.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment