Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Wales Chris
Coleman leo anataraji kukutana na
uongozi wa shirikisho la soka nchini humo kufanya mazungumzo ya kupewa mkataba
mpya wa kuendelea kuifundisha timu hiyo.
Coleman mwenye umri wa miaka 43 ambaye
mkataba wake wasasa unamalizika baada ya
mchezo wa kirafiki baina ya Wales na Finland tarehe 16 ya mwezi huu pia anahusishwa na mipango ya kujiunga na
timu ya Crystala Palace ya England.
Coleman ambaye alianza kuifundisha Wales
mwezi januari mwaka jana kuchukua nafasi
ya Gary Speed aliyefariki dunia mara
baada ya mazungumzo ya leo na uongoizi wa shirikisho la soka nchini humo
anatarajiwa kutangana kikosi cha timu ya taifa.
Akiwa kocha wa Wales Coleman amekiongoza
kikosi chake katika michezo 15 akishinda minne,kwenda sare miwili na kufungwa
michezo tisa huku akishindwa kuivusha nchi hiyo kwenye fainali zijazo za kombe
la dunia mwakani huko Brazil.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment