Pages

Ads 468x60px

Thursday, November 21, 2013

BODI YA WADHAMINI YA KLABU YA SIMBA YAPINGA MAAMUZI YA KUMSIMAMISHA RAGE NA BENCHI LA UFUNDI



Bodi ya wadhamini wa  klabu ya Simba imesema haitambui maamuzi yaliyotolewa na kamati ya Utendaji ya klabu hiyo kuhusiana na kumsimamisha mwenyekiti Ismail Aden Rage pamoja na benchi la ufundi.

Mwenyekiti wa baraza la wadhamini Hamisi Kilomoni amesema kuwa  wao kama bodi wamesikitishwa na hatua hiyo ya kamti ya Utendaji nakuongeza kuwa hawana barua juu ya mabadiliko hayo ya kumsimamisha rage.
Kilomini amsema wao hawaungi mkono migogoro  na kwamba wanachopenda  nikuona Simba ikiwa na maendleo mazuri  kwakuwa na uongozi wenye mshikamano wa dhati.

Amesema nia ya bodi hiyo ni kuijenga Simba na kuwakosoa wale wote wanaofanya maamuzi ya kukurupuka juu ya mambo mbalimbali ya klabuni mwao.

Kilomo hakusita kutangaza nia  na msimamo wa bodi hiyo  hiyo ya udhamini katika kuijenga Simba ambayo imeshindwa kuonyesha cheche zake katika duru ya kwanza ya ligi kuu Tanzania bara.
                                   
                             Posted by Yusup Mkule.

No comments:

Post a Comment