Pages

Ads 468x60px

Sunday, November 17, 2013

CAMEROON YAWA TIMU YA TATU KUFUZU KOMBE LA DUNIA KUTOKA BARANI AFRIKA,YAUNGANA NA NIGERIA NA IVORY COAST.


Timu ya taifa ya Cameroon imefanikiwa kufuzu fainali zijazo za kombe la dunia baada ya kuifunga Tunisia jioni ya leo magoli 4 kwa 1.

Ikicheza kwenye aridhi ya nyumbani Cameroon imepata magoli yake kupitia kwa Pierre Webo dakika ya 4 huku ya magoli mengine yakifungwa na Benjamin Moukandjo Bilé na Jean Makoun aliyefunga magoli mawili huku goli  la kufutia machozi kwa Tunisia likifungwa na  Ahmed Akaïchi.

Cameroon iliyokuwa ikiongozwa na nahodha wake Samweli Eto'o  ilicheza mchezo wa  kasi na nguvu nyingi jambo lililowawia vigumu wapinzani wao kufurukuta.

Katika mchezo wa awali mataifa hayo yalitoka suluhu ya bila kufungana  pambano ambalo Tunisia ilikuwa mwenyeji. Keshokutwa kutakuwa michezo  mingine ya kufuzu kwa kombe la dunia barani Afrika itachezwa siku ya jumanne ambapo Misri itaikaribisha Ghana huku Mbweha wa jangwani Algeria watakuwa wenyeji wa Burkinafaso.

                                                                              Posted by Yusuph Mkule.

No comments:

Post a Comment