Kuelekea katika mchezo wa kesho kati ya Manchester United na
Arsenal uongozi wa klabu ya Manchester umesema mshambuliaji Danny Welbeck
ataukosa mchezo huo kutokana na kupatwa na jeraha la goti.
Nyota huyo wa kimataifa wa England aliumia goti katika mchezo dhidi ya Fulham uliochezwa hivi karibuni na United kushinda magoli 3 kwa 1 .Pia jeraha hilo lilimfanya akose mchezo wa klabu bingwa Ulaya dhidi ya Real Sociedad mwanzoni mwa juma hili.
Kocha wa Manchester United, David Moyes amesema hilo ni pigo kwa klabu lakini anataraji kumtumia Robin Van Persi, Wayne na Javier Hernandez “Chicahrito” katika safu ya ushambuliaji.
Manchester United inayoshika nafasi ya 8 katika msimamo wa ligi kuu nchini England inataraji kuwakaribisha vinara wa BPL klabu ya Arsenal pambano linalotaraji kuchezwa majira ya saa 1 na dakika 10 usiku kwa saa za AfrikaMashariki hapo kesho.
Nyota huyo wa kimataifa wa England aliumia goti katika mchezo dhidi ya Fulham uliochezwa hivi karibuni na United kushinda magoli 3 kwa 1 .Pia jeraha hilo lilimfanya akose mchezo wa klabu bingwa Ulaya dhidi ya Real Sociedad mwanzoni mwa juma hili.
Kocha wa Manchester United, David Moyes amesema hilo ni pigo kwa klabu lakini anataraji kumtumia Robin Van Persi, Wayne na Javier Hernandez “Chicahrito” katika safu ya ushambuliaji.
Manchester United inayoshika nafasi ya 8 katika msimamo wa ligi kuu nchini England inataraji kuwakaribisha vinara wa BPL klabu ya Arsenal pambano linalotaraji kuchezwa majira ya saa 1 na dakika 10 usiku kwa saa za AfrikaMashariki hapo kesho.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment