Pages

Ads 468x60px

Thursday, November 28, 2013

IVO AIONGOZA KILI STARS KWENYE SARE NA CHIPOLOPOLO KATIKA MICHUANO YA CHALLANGE.






Timu ya taifa ya Tanzania bara Kilimanjaro stars leo imetoka sare ya kufungana goli 1 kwa 1 na timu ya taifa ya Zambia Chipolopolo kwenye mashindano ya kombe la Challenge yaliyoanza jana nchini Kenya.
Katika pambano hilo Zambia ndiyo iliyokuwa yakwanza kupata goli kupitia kwa mchezaji Ronald Kampamba  Dkk ya 41  Kabla ya Kili stars kusawazisha kunako dkk ya 48 likifungwa kwa kichwa na Said Morad.
Baada ya mchezo kumalizika kocha mkuu wa Kilimanjaro Stars Kim Poulsen amesema ameridhika na uwezo wa kikosi chake hivyo anamatumaini ya kufanya vyema michezo inayofuata.
Kim pia amesema wachezaji Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wanaoichezea TP Mazembe ya DRC Congo watakuwepo katika michezo inayofuata baada yah ii leo kukosekana kwenye kikosi hicho.
Naye kocha mkuu wa Chipolopolo mfaransa Patrice Beaumelle amezipongeza timu zote kwakucheza soka safi  huku akieleza matarajio yake kwenye michezo inayofuata kwakusema matokeo waliyoyapata ni mwanzo mzuri hivyo hanashaka yeyote na michezo inayofuata.
Kwaupande wake kiungo Salum Aboubakary wa Kili stars ambaye alichaguliwa nyota wa mchezo amesema kikosi chao kimecheza vibaya ungwe ya kwanza lakini kipindi cha pili walibadilika na hatimae kusawazisha goli na hatimae kupata sare hiyo.
Pia kiungo huyo ambaye ni mtoto wa nyota wa zamani wa klabu ya Yanga na timu ya taifa ya Tanzania Aboubakari Salumu “sure boy amelalamikia uwanja  wa Kenyatta uliopo Machakosi walioutumia leo kuwa haukua mzuri hasa baada ya mvua kunyesha.

Kwa matokeo hayo, Burundi inaongoza kundi hilo baada ya kuifunga Somalia 2-0 katika mchezo wa kwanza wa kundi hilo.
Kikosi cha Stars kilikuwa; Ivo Mapunda, Himid Mao, Erasto Nyoni, Said Morad, Kevin Yondan, Frank Domayo, Salum Abubakar ‘Sure Boy’/Ramadhani Singano ‘Messi’ dk89, Hassan Dilunga/Athumani Iddi ‘Chuji’ dk85, Elias Maguri/Haroun Chanongo dk72, Amri Kiemba na Mrisho Ngassa.

Chipolopolo; Nsabata Toaster, Bronson Chama, Jimmy Chisenga/Kabaso Chongo dk67, Christopher Munthali, Rodrcik Kabwe, Stanley Nshimbi/Alex Nshimbi dk57, Sydney Kalume, Kondwani Mtonga, Felix Katongo/Salulani Phiri dk73, Ronald Kampamba na Festus Ndewe.  

Kwenye mchezo wa awali hii leo Burundi ilifanikiwa kuifunga Somalia magoli 2 kwa 0

Kesho ni zamu ya Sudan na Eritrea kwenye uwanja wa Kenyata uliopo Machakosi majira ya saa nane kamili mchana wakati mabingwa watetezi Uganda wataikabili Rwanda kwenye uwanja huohuo wa Kenyatta saa kumi jioni.

mkule.blogspot.com

No comments:

Post a Comment