Pages

Ads 468x60px

Thursday, November 21, 2013

TIMU YA TAIFA YA URUGUAY YAFUZU KWENYE FAINALI ZA KOMBE LA DUNIA MWAKANI.




Timu ya taifa ya Uruguay imefanikiwa kuingia katika michuano ya kombe la dunia huko nchini Brazil mwaka 2014 baada ya kutoa suluhu na timu ya taifa Jordan.
Taifa hilo kutoka bara la Amerika ya kusini limekuwa ndio timu ya mwisho kufanikiwa kuingia katika mashindano hayo na kukamilisha idadi ya timu 32 kutoka mabara matano tofauti.
Katika mchezo wa kwanza uliochezwa nchini Jordan, Uruguay iliibuka na ushindi wa magoli matano kwa sifuri hivyo imepita kwa idadi hiyo ya magoli.
Uruguay ambao ni ni mabingwa wa dunia mara mbili inashika nafasi ya 6 katika orodha ya ubora wa shirikisho la soka duniani (FIFA) walifika hatua ya nusu fainali katika kombe la dunia mwaka 2010 lililofanyika nchini Afrika ya kusini.
                        Posted by Yusuph Mkule.




Golikipa wa timu ya taifa ya Hispania na klabu ya FC Barcelona Victor Valdes amepata jeraha la msuli litakalomuweka nje ya uwanja kwa mudawa mwezi mmoja na wiki mbili.
Valdes amepata jeraha hilo katika mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya taifa ya Afrika ya kusini ikiwa ni dakika 25 baada ya kuchukua nafasi ya Iker Cassilas.
Mhispania huyo ameshacheza michezo 19 msimu huu katika klabu ya Barcelona na ameshatangaza kuwa anataraji kuihama klabu hio mwishoni mwa msimu wa mwaka 2013/2014.
Valdes anataraji kukosa michezo miwili ya klabu bingwa Ulaya na miwili ya ligi kuu nchini Hispania (La Liga) huku akitizamiwa kurudi mwezi wa kwanza mwaka 2014.
           

                      Posted by Yusuph Mkule.


 Mlinzi wa timu ya Liverpool kufanyiwa upasuaji wa goti linalomsumbua………………
Kocha mkuu wa klabu ya Liverpool Brendan Rodgers amethibitisha kuwa mlinzi  wa timu hiyo Jose Enrique anahitajika kufanyiwa upasuaji  wa goti kutokana na jeraha alilonalo.
Rodgers  ambaye kikosi chake kimeanza vyema msimu huu wa ligi amebainisha kwamba  raia huyo wa Hispania anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu kutokana na upasuaji atakaofanyiwa.
Mchezaji huyo ambaye aliumia kwenye pambano la timu yake ya Liverpool na Manchester United mwezi wa tisa mwaka huu alirejea uwanjani mwanzoni mwa mwezi huu na kucheza pambano dhidi ya Fulham ambapo Liver ilishinda magoli 4 kwa 0.
Kwasasa kikosi cha Liverpool kinashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi kikiwa na alama 23 nyuma ya Arsenal ambayo inaoongoza kwa alama 25.

                          Posted by Yusuph Mkule.


Timu ya soka ya AS Roama ya Italia imeingia  kwenye kinyang’anyiro cha kutaka kumsajili  nyota wa Fc Lille ya Urafansa Solomon Kalou ambae pia anawaniwa na vinara wa ligi kuu ya England Arsenal.
Kwamujibu wa  gazeti mmoja barani Ulaya  kocha Rudi Garcia amenukuliwa akisema yupo kwenye mipango ya kuimarisha kikosi chake cha  Roma kwenye msimu wa usajili mwezi januari mwakani baada ya kuanza vyema msimu huu wa ligi ya Italia.
Roama ambayo haijafungwa michezo 12 ya ligi msimu huu na kushinda mipambano 10  wanauwezekano wa kumsajili raia huyo wa Ivory Coast  ambaye alijiunga na Lille akitokea Chelsea ya England kutokana na uwezo alionao.
Kalou ambaye anaumri wa miaka 28 hivi karibuni amefunga goli la 23 katika timu ya taifa kwenye mchezo dhidi ya Senegal uliomalizika kwa sare ya goli 1 kwa 1na hatimae kufuzu fainali za kombe la dunia zitakazofanyika nchini Brazil mwakani.
                     Posted by Yusuph Mkule.




No comments:

Post a Comment