Pages

Ads 468x60px

Sunday, November 10, 2013

WENGER AJIVUNIA KIKOSI BORA ALICHONACHO KITAKACHOIANGAMIZA MACHESTER UNITED LEO.





Kocha wa klabu ya Arsenal raia wa Ufaransa Arsene Wenger anaamini kuwa kikosi chake alichokijenga kwa vijana wengi kitaiadhibu Manchester United hii leo kwenye mchezo wa ligi kuu ya England unaotaraji kuchezwa  milango ya saa 1 na dakaka kumi usiku wa leo Old Traford.
Mfaransa huyo anayejifunia mwenendo mzuri walioanza nao msimu huu kwenye ligi kiasi cha kushikilia usukani hadi sasa anakifananisha kikosi chake na kile cha Man United cha mwaka 1992  kilichotwaa ubingwa wa tano wa ligi kuu ya England.
Wenger amewataja wachezaji wa Manchester United mwaka huo wa 1992  kama Ryan Giggs,Paul Schole,Nick Butt,David Bekham  kwamba ni kati ya kikosi anachoamini kilikuwa bora sana kwa United kama Arsenal ya sasa aliyoijenga kwa muda mrefu.
Wenger ametaja wachezaji wake vijana anaoamini kwa umri wao hakuna wa kuwazuia kufanya vyema simu huu hatimae kutwaa ubingwa.
Amewataja wachezaji  Aaron Ramsey, miaka 22, Jack Wilshere, 21, Theo Walcott, 24, Alex Oxlade-Chamberlain, 20, Kieran Gibbs, 24, na Wojciech Szczesny miaka 23 kwamba kwa uwiano wa umri wao wanauwezo wa kuisaidia Arsenal kwa kiasi kikubwa.


Wenger anajifunia  safu nzuri ya ushambuliaji aliyonayo ikiongozwa na Aaron Ramsey aliyefunga magoli 11 msimu huu likiwemo goli alilowafunga Borussia Dortmund kwenye michuano ya klabu bingwa Ulaya juma hili.

Arsenal inaikabili Man United kwenye uwanja wa Old Traford ikiwa  inaongoza ligi kwa alama  25 huku United ikiwa na alama 17 ikiwa ni tofauti ya alama 8 timu zote zikiwa zimecheza michezo 10 pekee.


Hii ni sehemu ya kikosi cha Machester United kilichotwaa ubingwa wa ligi kuu ya nchini England mwaka 1992.



Matumani ya Wenger yapo kwa hawa vijana hii leo pale Old Traford. 

                      Posted by Yusuph Mkule.


No comments:

Post a Comment