Klabu ya soka ya Marseille ya
Ufaransa imetangaza kuwa nyota wake raia wa Ghana Andre Ayew amefanyiwa upasuaji wa goti lake lililokuwa
linamsumbua na upasuaji huo umeenda salama.
Ayew ambaye aliitumikia Ghana kwenye mchezo wa play off
kufuzu kombe la dunia wiki iliyopita dhidi ya Misri upasuaji wake umefanyika jana chini ya daktari
Jean-Piere Francesnch na anatarajiwa kutoka hospitalini kesho.
Taarifa hiyo imearifu kuwa raia huyo
wa Ghana anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa muda wa miezi 2 na anatarajiwa
kurejea uwanjani mwezi January mwakani.
Ayew
akiwa na kikosi cha Marseille msimu huu wa ligue one amefunga magoli 8 katika michezo 9 aliyocheza
huku akiwa amecheza kwa kusuasua kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya goti.
mkule.blogspot.com
No comments:
Post a Comment