Pages

Ads 468x60px

Sunday, November 24, 2013

RAGE AKAIDI AGIZO LA TFF LAKUMTAKA AITISHE MKUTANO NDANI YA SIKU 14 KUANZIA JANA.






Mwenyekiti wa klabu ya Simba Ismail Aden  amesema kuwa yupo tayari kujiuzuru nyazifa yake kuliko kuitisha mkutano wa wanachama siku kumi na nne zilizotolewa na Uongozi wa Shirikisho la soka nchini TFF.
Rage amekaidi  amri hiyo leo baada ya  uongozi wa Shirikisho la soka nchini TFF kupitia kwa  Rais wake Jamal Malinzi kuwa aitishe  mkutano ndani ya siku 14 kuanzia jana.
Amesema hayupo tayari kuvunja katiba ya Tff na ya Simba kwashinikizo la watu wachache wanaotumiwa kuivuruga Simba tena mbaya zaidi anapangiwa muda na ajenda za mkutano huo kitu ambacho hakipo kwenye katiba ya Simba na ya TFF.
Rage amesema hataitisha mkutano wowote  ndani ya Simba na ataendelea na madaraka yake kama kawaida ya kuiongoza klabu hiyo.
 Aidha Rage ameiomba TFF iheshimu katiba ya Simba ili uongozi wa timu hiyo ufanye kazi ya kutekeleza majukumu yao.
Wakati huohuo, Mwenyekiti wa Simba Ismail Aden ameteuwa Michael Wambura kuwa mjumbe wa kamati ya utendaji, huku Rahma Alharoos  malkia  wa nyuki wamemuomba awe mdhamini wa klabu hiyo.
 Hata hivyo amesema tuhuma anazopewa kuhusu kula  pesa za mchezaji wake wa zamani  Emanuel Okwi  sio za kweli kwakuwa usajili huo hakutangazia chumbani na mke wake aliutangazia umma wa Tanzania na kila mtu alisikia.

                             Posted by Yusuph Mkule.

No comments:

Post a Comment