Mlinda mlango wa vinara wa ligi kuu
ya nchini England Arsenal Wojciech
Szczesny amesaini mkaba mpya utakaomfanya aendelee kuvaa uzi wa The Gunners kwa kipindi kirefu zaidi.
Raia huyo wa Poland mwenye umri wa
miaka 23 tangu ajiunge na Arsenal akitokea Legia Warsaw mwaka 2006 ameichezea Arsenal michezo 123 huku akidakia timu ya taifa lake kwa mara ya
kwanza mwezi September mwaka 2009.
Szczesny ambaye ni mtoto wa golikipa
wa zamani wa timu ya taifa ya Poland Maciej
Szczesny hata hivyo mkataba wake
huo haujawekwa wazi utaisha lini lakini kocha wa Arsenal amemzungumzia nyota huyo kuwa anakipaji kikubwa ndiomaana
wamerefusha mkataba wake.
Mchezaji huyo ambaye amekuwa
Tengemeo kwa Arsenal inayoongoza ligi kwa alama
25 msimu huu hadi sasa amesema anajivunia kuwa mchezaji wa Arsenal na
anandoto kubwa ya kupatia mafanikio timu hiyo.
Mchezaji huyo aliichezea Poland
mchezo wa 15 mwezi oktoba mwaka huu kwenye uwanja wa Wembley ambapo ilikuwa
ikicheza na England kutafuta tiketi ya kucheza kombe la dunia mwakani.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment