Kocha wa timu ya taifa ya Brazil Luiz Felipe
Scolari amesema kuwa anapenda kufundisha soka nchini England licha ya kuudhiwa
alipokuwa anaifundisha Chelsea mwaka 2008.
Scolari ambaye alidumu kwa muda wa miezi saba
alipokuwa kocha wa Chelsea amesema alipenda kuifundisha timu hiyo kwa misimu
miwili au zaidi kutokana na alivyokuwa
akiijenga timu hiyo lakini alisikitishwa na uamuzi wa kufukuzwa na mmiliki wa
timu hiyo.
Scolari ambaye kwasasa anaifundisha Brazil yenye wachezaji
wengi Chipkizi ameongeza kuwa uamuzi wa kufukuzwa na tajiri wa Chelsea Roman
Abromovic haukuwafurahisha wachezaji wengi
kwenye kikosi alichokuwa akikifundisha.
Hatahivyo Scolari amesema kama atapata nafasi
ya kurudi England angependa akaifundishe
Chelsea kwakuwa bado anahitaji kuipa
mafanikio mazuri timu hiyo yenye makao makuu yake magharibi mwa jiji la London.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment