Baada ya
kuiongoza Mbeya City na kumaliza duru ya kwanza ya ligi kuu ya soka Tanzania bara
kocha mkuu wa timu hiyo Juma Mwambusi
amewashukuru wadau na mashabiki
kwakuwaunga mkono kwenye michezo yote ya nyumbani na ugenini.
Mwambusi
amesema ushirikiano mkubwa walioupata kutoka kwa mashabiki na wadau umechangia wao kumaliza duru hii
bila kufungwa huku wakishika nafasi ya tatu kwenye msimamo nyuma ya Yanga na
Azam fc.
Aidha kocha
huyo amesema hatarajii kusajili mchezaji nje ya kikosi chao kwenye msimu wa
usajili kabala ya duru ya lalasalama
kuanza mwezi wa kwanza mwakani.
Amesema kama
atahitaji kukiongeza nguvu kikosi chake atatumia wachezaji wengine waliyopo
kwakuwa anaamini timu hiyo inayoshiriki VPL kwa mara ya kwanza inawachezaji
wengi na wazuri.
Pia Mwambusi
amesema mara baada ya mapumziko mafupi
timu hiyo itaanzaa maandalizi ya duru ya mwisho kwa kucheza michezo mingi ya
kirafiki kwalengo la kutwaa ubingwa wa ligi kuu Tanzania bara msimu huu wa
2013/2014.
Katika duru ya lala salama Mbeya City itaanza kwakusafiri hadi mkoani Kagera kuifuata
Kagera Sukari januari 24 mwakani pambano litakalochezwenye uwanja wa Kaitaba.
Posted by Yusuph Mkule.
Posted by Yusuph Mkule.
No comments:
Post a Comment