KOCHA Muingereza, Stewart Hall
atakuwa Kocha Mkuu wa akademi ya Symbion Power inayoanzishwa nchini kwa
ushirikiano wa klabu ya Sunderland AFC ya England na Wizara ya Habari Utamaduni
na Michezo.
Mtendaji Mkuu wa Symbion Power Tanzania, Peter Gathercole, amesema leo kwamba akademi hiyo itakuwa na vituo Kidongo Chekundu (Sports Park) na Elite Football Academy, Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Symbion Power Tanzania, Peter Gathercole, amesema leo kwamba akademi hiyo itakuwa na vituo Kidongo Chekundu (Sports Park) na Elite Football Academy, Dar es Salaam.
Kabla ya hapo, Hall alikuwa kocha wa
timu za taifa za Saint Vincent na Grenadines, pamoja na Pune FC ya India.
Akizungumza jana mjini Dar es Salaam, Hall alisema, “Mradi huu hakika utasaidia kuinua soka ya vijana kwa viwango vyote, timu za taifa na klabu. Vijana wadogo watafundishwa ufundi, mbinu, kujengewa uimara wa kimchezo na maarifa ya soka ya kisasa,”alisema.
Mtendaji Mkuu wa Sunderland AFC, Margaret Byrne, amesema: “Tunafurahi mradi wa akademi unaendelea vizuri. Kuteuliwa kwa Stewart ni hatua ya kufurahisha na tunatarajia kila mmoja kufanya kazi kwa bidii ili kuvuna matunda baadaye.”
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara, alitemebelea akademi ya Sunderland akiwa ameambatana na Rais Jakaya Kikwete Juni mwaka huu ambako walifikia makubaliano na Sunderland AFC na Symbion Power Tanzania juu ya mradi huu.
Akizungumza jana mjini Dar es Salaam, Hall alisema, “Mradi huu hakika utasaidia kuinua soka ya vijana kwa viwango vyote, timu za taifa na klabu. Vijana wadogo watafundishwa ufundi, mbinu, kujengewa uimara wa kimchezo na maarifa ya soka ya kisasa,”alisema.
Mtendaji Mkuu wa Sunderland AFC, Margaret Byrne, amesema: “Tunafurahi mradi wa akademi unaendelea vizuri. Kuteuliwa kwa Stewart ni hatua ya kufurahisha na tunatarajia kila mmoja kufanya kazi kwa bidii ili kuvuna matunda baadaye.”
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara, alitemebelea akademi ya Sunderland akiwa ameambatana na Rais Jakaya Kikwete Juni mwaka huu ambako walifikia makubaliano na Sunderland AFC na Symbion Power Tanzania juu ya mradi huu.
KIKAO CHA KWANZA JUU YA UKARABATI WA DIMBA LA SOKOINE JIJINI MBEYA CHAFANYIKA.
Katibu mkuu wa timu hiyo
Emanueli Kimbe amesema leo novemba 14 wamekutana na wamiliki wa uwanja huo sambamba
na chama cha soka mkoani humo kujadili chakufanya.
Amesema katika kikao hicho
kilichohudhuriwa na wawakilishi wa timu ya Tanzania Prisons ya mkoani humo
wamejadiliana kwa pamoja na kutoka na kauli ya pamoja kuwa watashirikiana
kufanya ukarabati huo.
Hata hivyo ukarabati juu
ya dimba hilo unataraji kuanza mara baada ya kufanyika kwa kikao cha wamiliki
wa uwanja huo siku ya jumapili na majibu
juu ya ni lini na jinsi gani ukarabati huo utafanyika yatatolewa juma
lijalo.
Katika hatua nyingine
Kimbe amezionya timu ambazo zinampango wa kuwahadaa wachezaji wao katika msimu
huu wa usajili kwa dirisha dogo kuacha mara mmoja harakati zao kwasababu Mbeya
City haina mpango wa kuuza mchezaji yeyote.
Pia amesema kama kuna timu
inahitaji mchezaji ni vyema ikaonana na uongozi badala ya kuonana na mchezaji
wanaomtaka kwakuwa kufanya hivyo ni kosa.
Posted by Yusuph Mkule.
Uongozi wa chama cha mpira mkoa wa
Iringa leo umetoa ufafanuzi juu ya kujitoa kwa timu soka ya Nyang’oro iliyokuwa
ikishiriki ligi ya mkoa inayoendelea kutimua vumbi mkoani humo.
Katibu mkuu wa chama hicho Eliud
Mvela mbali na kutoa ufafanuzi wa timu hiyo kujiondoa amezungumzia suala ya
timu mbalimbali ambazo hazijashiriki ligi hiyo msimu huu kwasababu ya kutokuwa
na imani na uongozi wa IRFA.
Amesema timu ya Nyang’oro
imewasilisha barua ikiomba kujitoa kutoaka na wachezaji wake wengi
kujishughulisha na masuala ya kilimo msimu huu hivyo hawawezi kushiriki
kikamilifu.
Katika hatua nyingine Mvela amesema malalamiko yanayotolewa na vilabu
ambavyohavijashiriki ligi hiyo msimu huu kutokana na kutofautiana na uongozi wa
chama cha mpira sio sahihi.
Amesema ligi inaendeshwa kwa umakini
mkubwa na vilabu vinavyokilalamikia chama cha mpira madai yao hayana ukweli wowote.
Timu za Sengo,Bbc Fc ,Home Boys na
Kilolo fc zimejiondoa kushiriki ligi ya mkoa wa Iringa msimu huu kwakulalamikia
maamuzi mabaya yanayofanya na waamuzi huku chama cha mpira mkoa kikilalamikiwa
kuhusika na timu hizo kuonewa kila msimu wa ligi unapo anza.
No comments:
Post a Comment