Mikel Arteta aliyekaa chini,hapa ilikuwa katika mchezo dhidi ya Borussia Dortmund.
Mathieu Debuchy akiwa katika mmoja ya mikikimikiki na kikosi cha Arsenal.
Klabu ya soka ya Arsenal
imepata pigo kubwa baada ya wachezaji wake Mikel Arteta na Mathieu Debuchy
kulazimika kuwa nje ya Uwanja kwa Miezi Mitatu baada ya kufanyiwa upasuaji.
Arteta
mwenye Miaka 32, amefanyiwa upasuaji wa kifundo cha mguu baada ya kuumia muda
mrefu wakati Debuchy amefanyiwa upasuaji kwenye Bega aliloumia juma lililopita.
Mara baada
ya kujiunga na Arsenal mwanzoni mwa Msimu akitokea newcastle, Debuchy aliumia
na kuwa nje kwa Miezi Mitatu na hali
hiyo imemfanya aichezee Arsenal michezo 14 tu .
Arteta,
ambae mara ya mwisho kuichezea Arsenal ni Novemba 26 ilipoifunga Borussia
Dortmund magoli 2-0, amefunga magoli 16 katika Michezo 136 aliyoichezea Arsenal
tangu ajiunge nayo akitokea Everton Agosti 2011.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment