Pages

Ads 468x60px

Sunday, August 17, 2014

BAADA YA KIPIGO WENYE MAN YAO WAANZA KUMTAHADHARISHA VAN GAAL.




                                        Van Gaal akiwa na msaidizi wake Ryan Giggs

Kiungo wa zamani wa Manchester United Paul Scholes amesema timu hiyo inahitaji kufanyiwa mabadiliko makubwa kama inataka kushiriki michuano ya klabu bingwa Ulaya msimu ujao.
Akizungumza baada ya Manchester United kufungwa magoli 2 kwa 1 kwenye mchezo wake wa kwanza wa ligi kuu ya England hapo jana dhidi ya Swansea City Scholes amesema  ipo haja ya kocha mkuu Lous Van Gaan kukiimarisha zaidi kikosi chake.
Mkongwe huyo ambaye aliichezea United kwa mafaikio makubwa enzi zake amesema baada ya kuondoka kwa Nemanja Vidic,Patrice Evra  na Rio Ferdinand Van Gaal alipaswa kusajili wachezaji  wazoefu wa nafasi hizo na sio kama alivyofanya.
 Scholes amesema wachezaji Tony Kroon aliyejiunga na Real Madrid akitokea Bayern Munich na Cesc Fabrigas aliyejiunga na Chelsea akitokea Barcelona walikuwa sahihi kwa Manchester United.
Kauli ya nyota huyo liyeichezea United michezo 700 inamaanisha kama kocha Louis Van Gaal hatotumia vyema muda uliobaki wa usajili barani Ulaya kwakununua wachezaji atakuwa na wakati mgumu kufuzu klabu bingwa Ulaya  msimu ujao.

MATOKEO YA MICHEZO YA JANA BPL HAYA HAPA. 





LEO TAREHE 17.08.2014.

Liverpool vs Southampton.saa 15:30

Newcastle United vs Manchester City saa 18:00

                         Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment