Loic Remy.
Klabu ya soka ya Queens Park
Rangers imeahidi kumpa mkataba mpya mshambuliaji wake Loic Remy ambaye hivi
karibuni alishindwa kufaulu vipimo vya afya kujiunga na timu ya Liverpool.
Remy mwenye umri wa miaka 27
kwasasa yupo kwenye mazungumzo ya
kupatiwa mkataba mpya lakini jambo hilo linatarajiwa kufanyika mara baada ya
dirisha la usajili barani Ulaya kufungwa
siku ya jumatatu ijayo.
Kocha wa QPR Harry Redknapp
amemwanzisha mshambuliaji huyo raia wa Ufaransa katika michezo miwili ya awali
ya ligi kuu ya England ambapo timu hiyo
ilipoteza yote kwakufungwa na Hull City na Tottenham hot spurs.
Licha ya vilabu kadhaa
kuendelea kuonyesha nia ya kumsajili nyota huyo ikiwemo Newcastle United kocha Harry Redknapp amebainisha kuwa hadi kufikia septemba mosi mchezaji huyo
atakuwa amesaini mkataba mpya.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment