Rais wa timu
ya PSG Nasser Al-Khelaifi.
Mabingwa
wa ligi kuu ya Ufaransa PSG wamejiondoa katika mbio za kuwania sahihi ya nyota
wa Real Madrid ya Hispania Angel Di Maria ambaye kwa majuma kadhaa wamekuwa
kwenye mazungumzo.
Rais wa timu
hiyo Nasser Al-Khelaifi ametangaza rasmi kujiondoa katika vita ya kutaka
kumsajili nyota huyo raia wa Argentina kwakile alichoeleza anauzwa bei kubwa na
hawawezi kumtwaa.
Al-Khelaifi
amebainisha kuwa baada ya kufanya mazungumzo na rais wa Real Madrid Florentino
Perez wameshindwa kufikia muafaka kuuziana mchezaji huyo kutokana na dau
wanalolitaka kuwa kubwa na hawana budi kusitisha majadiliano hayo.
Tayari PSG
chini ya kocha wake mkuu Laurent Blanc imesha msajili mlinzi wa kibrazil David
Luiz kutoka Chelsea kwakiasi cha Euro milioni 50 msimu huu na pia imemsajili
Serge Aurier kwa mkopo kutoka Toulouse.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment