Mchezaji wa mchezo wa gofu
Tiger Wood ametangaza kutoshiriki mashindano ya kombe la Ryder ambayo
yanatarajiwa kuanza mwezi ujao nchini Scotland.
Tiger mwenye umri wa miaka 38 anayechezea
timu ya taifa ya Marekani amekuwa akisumbuliwa mara kwa mara na maumivu ya
mgongo ambayo yalimsababishia kufanyiwa upasuaji mapema mwezi wa tatu mwaka
huu.
Ameongeza kuwa anasikitishwa
kushindwa kujiunga na kikosi hicho kwani alipanga kutetea nchi yake katika
mshindano hayo ya Ryder ambayo yanataraji kuanza tarehe 23 hadi 28 mwezi ujao
nchini Scotland.
Hata hivyo nyota huyo wa mchezo
wa gofu amemuomba radhi kocha wa timu ya taifa ya mchezo huo Tom Watson kuwa hatoweza kushiriki
mashindano hayo kutokana na wataalamu wake wa afya kumtaka apumzike kwanza ili
aweze kupona vizuri.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment