Angel di maria.
Uongozi wa Manchester United umefikia makubaliano na Real Madrid juu ya kumsajili mshambuliaji Angel di Maria kwa ada ya paundi milioni sitni na tatu nukta tisa uliovunja rekodi ya uhamisho nchini England.
Kwamujibu wa kituo cha Sky Sport Di Maria mwenye umri wa miaka 26 raia wa Argentina anatarajiwa kusafiri leo kuelekea jijini Manchester kukamilisha taratibu za kujiunga na mabingwa hao mara 20 wa ligi kuu ya England huku ikielezwa upo uwezekano mkubwa wa kupewa jezi namba 7 iliyowahi kuvaliwa na wachezaji mbalimbali maarufu walioichezea timu hiyo kama C.Ronaldo,David Bekham na wengineo.
Kocha mkuu wa Real Madrid Carlo Ancelotti jana jumapili amethibitisha kuwa Di Maria aliwasili kwenye mazoezi ya timu hiyo kwaajili ya kuwaaga wachezaji wenzake pamoja na wafanyakazi wengine wa mabingwa hao wa Ulaya kwa vilabu.
Pia kiungo wa Real Madrid Xabi Alonzo amemtakia mafanikio mema dimaria kwakuandika kupitia ukurasa wake wa twiter kukumwambia daima hatosahaulika Santiago Bernabeu kutokana na mchango mkubwa alioutoa akiwa klabuni hapo.
Kwa upande mwengine kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti amesema mchezaji Sami Khedira hatoondoka klabuni hapo msimu huu na tayari uongozi wa timu hiyo umemhakikishia kwamba atabaki.
REKODI YA USAJILI KWA KLABU ZA UINGEREZA. |
|||
2011 | Fernando Torres | £50m | Liverpool to Chelsea |
2013 | Mesut Ozil | £42.4m | Real Madrid to Arsenal |
2011 | Sergio Aguero | £38m | Atletico Madrid to Manchester City |
2014 | Juan Mata | £37.1m | Chelsea to Manchester United |
2011 | Andy Carroll | £35m | Newcastle to Liverpool |
2014 | Alexis Sanchez | £35m | Barcelona to Arsenal |
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment