Mhambuliaji mkongwe wa timuu ya taifa ya Ivory Coast na klabu ya Chelsea Didier Drogba atangaza kustaafu kuitumikia timu yake ya taifa baada ya kuitumikia kwa miaka 12.
Drogba mwenye umri wa miaka 36 hivi
asasa amefunga magoli 65 katika michezo 104 aliyoichezea timu ya taifa ya Ivory
Coast na fainali za kombe la dunia mwaka huu zilikuwa za mwisho kwenye historia
ya maisha yake ya soka.
Akizungumza baada ya uamuzi wake wa
kustaafu Drogba ameandika kwenye ukurasa wake wa Twita kuwa anajisikia huzuni
sana hasa ikizingatiwa amelitumikia taifa lake kwa miaka 12.
Drogba ambaye msimu huu amesajiliwa kwa mara nyingine na Chelsea na kusaini mkataba wa mwaka mmoja amesema anajivunia kuwa nahodha wa timu ya taifa kwa miaka minane na kwa muda huo ameshiriki kombe la dunia mara 3,kuiwezesha nchi hiyo kufuzu fainali za AFCON mara 2.
Drogba ambaye msimu huu amesajiliwa kwa mara nyingine na Chelsea na kusaini mkataba wa mwaka mmoja amesema anajivunia kuwa nahodha wa timu ya taifa kwa miaka minane na kwa muda huo ameshiriki kombe la dunia mara 3,kuiwezesha nchi hiyo kufuzu fainali za AFCON mara 2.
Mchezo wa kwanza wa droba kuichezea timu
ya taifa ya Ivory Coast ulikuwa dhidi ya Afrika ya kusini September mwaka 2002.
Drogba
kwa mara ya kwanza kucheza kombe la dunia ilikuwa mwaka 2006 na kufunga
goli kwenye pambano la ufunguzi dhidi ya Argentina ambapo timu
yake ilifungwa magoli 2 kwa 1.
Drogba pia akacheza tena fainali za kombe la dunia mwaka 2010 lakini hakufunga goli lolote katika michezo mitatu aliyocheza na hata katika fainali za mwaka huu Tembo hao wa Ivory Coast wameshindwa kufurukuta baada ya kutolewa hatua ya makundi.
Drogba pia akacheza tena fainali za kombe la dunia mwaka 2010 lakini hakufunga goli lolote katika michezo mitatu aliyocheza na hata katika fainali za mwaka huu Tembo hao wa Ivory Coast wameshindwa kufurukuta baada ya kutolewa hatua ya makundi.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment