Mshambuliaji
wa mabingwa wa ligi kuu ya England Manchester City Sergio Aguero amerefusha
mkataba wake kwakuongeza miaka mingine mitano ya kuendelea kuichezea timu hiyo
yenye maskani yake jijini Manchester.
Aguero
mwenye umri wa miaka 26 mkataba wake mpya aliyeuongeza utamfanya aendelee
kuitumikia klabu hiyo hadi mwaka 2019
tangu ajiunge nayo mwaka 2011 akitokea kwa mabingwa wa La Liga Atletico
Madrid.
Raia huyo wa
Argentina tangu ajiunge na City amefunga
magoli 75 katika michezo 122 aliyocheza
na kuongeza kwake mkataba
mpya kumefuta uvumi uliyoanza
kuzagaa kuwa nyota huyo anampango wa kuihama timu hiyo.
Akizungumza mara baada ya kusaini mkataba huo Aguero amesema najisikia furaha kuitumikia timu pekee yenye ushirikiano mkubwa kuanzia mashabiki,wachezaji na viongozi na hilo ndilo lililofanya wawe na mafanikio makubwa.
Akizungumza mara baada ya kusaini mkataba huo Aguero amesema najisikia furaha kuitumikia timu pekee yenye ushirikiano mkubwa kuanzia mashabiki,wachezaji na viongozi na hilo ndilo lililofanya wawe na mafanikio makubwa.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment