Eliaquim Mangala.
Mabingwa wa ligi kuu ya England timu ya Manchester city
wametangaza rasmi kumsajili mlinzi wa kifaransa Eliaquim Mangala kutoka Fc
Porto ya Ureno kwa uhamisho wa Euro milioni 40.
Mangala
ambaye alikamilisha vipimo vya Afya mwezi july
mara baada ya kukamilisha uhamisho huo amesema anajisikia furaha kuhamia
Manchester City kwakuwa ni mmmoja ya vilabu vikubwa barani Ulaya na
anamatumaini ya kuendeleza kipaji chake.
Mangala amesema lengo lake kuu la kujiunga na Manchester City ni kutwaa mataji mbalimbali na huku akiisifu ligi kuu ya England ni kati ya ligi bora duniani na yenye ushindani mkubwa sana.
Mangala amesema lengo lake kuu la kujiunga na Manchester City ni kutwaa mataji mbalimbali na huku akiisifu ligi kuu ya England ni kati ya ligi bora duniani na yenye ushindani mkubwa sana.
Mangala
amekuwa mchezaji wa 6 kujiunga na Manchester City msimu huu wa usajili
akiungana na nyota wengine watano ambao ni Sagna, Fernando, Willy Caballero, Frank
Lampard na Bruno Zuculini.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment