Mashabiki wa timu ya taifa ya Ghana.
Nchi ya Ghana imetuma ombi la
kuandaa fainali za kombe la mataifa ya Afrika mwaka 2017 baada ya Libya kujitoa juma lililopita kuwa mwenyeji kutokana na hali ya kisiasa
ilivyo hivi sasa kwenye taifa hilo la
kaskazini mwa Afrika.
Ombi la Ghana kutaka kuandaa fainali
hizo linatokana na tangazo lililotolewa jumanne
iliyopita na shirikisho la soka barani Afrika CAF na mwisho wa kupokea maombi hayo ni
September 30 mwaka huu.
Uongozi wa shirikisho la mpira nchini Ghana
umethibitisha kupewa baraka zote na serikali yao kutuma ombi hilo kupitia kwa mwaklishi wa rais wa taifa hilo
John Dramani na kusema wanamatumaini
makubwa ya kupewa heshima ya kuandaa michuano hiyo.
Ghana inaungana na mataifa kadhaa yaliyomba nafasi hiyo ya kuwa
mwenyeji wa fainali hizo za mwaka 2017,nchi nyingine ni Kenya,Tanzania na Rwanda ambazo tayari zimeshawasilisha maombi yao
CAF.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment