Nyota wa mabingwa wa ligi kuu
ya Ufaransa Zlatan Ibrahimovic amekanusha
habari zilizozagaa zakusema anampango wa kurudi katika timu ya Juventus ambao
ni mabingwa wa ligi kuu ya Italia Serie A.
Zlatan ambaye ni raia wa Swiden
amesema hamjui mtu aliyejitambulisha kwa jina la Stefan Hansson aliyekaririwa
na vyombo vya habari akisema kwamba yeye anampango wa kurudi Italia kuichezea
timu ya Juventus.
Hansson hivi karibuni
alikaririwa na baaadhi ya vyombo vya habari barani Ulaya akisema anaurafiki wa
karibu na nyota huyo tangu alipokuwa akiichezea Malmo na kwamba anauhakika wa
Zlatan kurudi Italia lakini nyota huyo amekana kumtambua.
Ibrahimovic ambaye alifunga
magoli mawili mwishoni mwa juma lililoisha jana
dhidi ya Reims ambapo pambano hilo lilimalizika kwa sare ya magoli 2 kwa
2 mkataba wake na PSG unamalizika mwezi
wa sita mwaka 2016.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment