Mlinzi wa
klabu ya Olympiakos ya Ugiriki Kostas Manolas
anajiandaa kwenda kufanyiwa vipimo vya afya tayari kwa kujiunga na timu
ya Arsenal inayoshiriki ligi kuu ya England kuziba nafasi ya Thomas Vermaelen
aliyejiunga na Fc Barcelona.
Imeripotiwa
kuwa Arsenal ilianza mazungumzo na Olympiakos mapema mwezi huu na pande hizo
mbili zinaelezwa kufikia makubaliano ya kuuziana mchezaji huyo kwa uhamisho wa
Euro milioni 10.
Hivi
karibuni kocha wa Arsenal mfaransa Arsene Wenger alikaririwa akisema atafanya usajili wa nafasi ya ulinzi wakati
licha ya kumsajili Calum Chambers kwa ada ya Euro milioni ishirini.
Arsenal
ambayo jana ilipata ushindi wa magoli 2 kwa1 ikiwa nyumbani dhidi ya Crystal Palace pamoja na kuwa kwenye nafasi nzuri ya
kumsajili Kostas Manolas nayo
timu ya Juventus ya Italia imeonyesha nia ya kumtaka mchezaji huyo.
Mkule.blogsports.com
No comments:
Post a Comment