Mlindamlango
Pepe Reina leo ijumaa anataraji kusainikataba na maabingwa wa ligi kuu ya
ujerumani Bundesiliga Fc Bayern Munich baada ya kufaulu vipimo alivyofanyiwa
jana Alhamisi.
Tayari uongozi
wa Bavarian umethibitisha kupitia ukurasa wao wa Twiter kuwa Reina atasaini
mkataba huo leo ijumaa baada ya klabu
yake ya Liverpool kufikia makubaliano na kikosi hicho kinachofundishwa na kocha
Pep Guadiola.
Reina alijunga
na Liverpool mwaka 2005 mwezi julai na kushinda kombe la FA ,kombe la ligi
kwa muda wote akiwa na vijogoo hao wa
Anfield.
Pamoja na kucheza kwa mkopo msimu uliopita kwenye klabu ya Napoli ya Italia
Reina amepoteza nafasi ya kuwa golikipa namba moja wa Liverpool kutokana na
mlinda mlango wa sasa Simon Mignolet kuaminiwa zaidi na kocha mkuu Brendan
Rogers.
Akiwa
Beryen munich Reina anatarajiwa kuwa mlinda mlango namba mbili nyuma ya Manuel Neuer pale Allianz Arena mjini
Munich
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment