Pages

Ads 468x60px

Friday, August 22, 2014

NI APR (APEREE) NA EL MEREKH FAINALI YA KAGAME 2014 KESHO MJINI KIGALI RWANDA.



 Mlindamlango wa El merekh Salim Omar Magoola, mwenye umri wa miaka 21 aliyeibuka shujaa kwa kuokoa mikwaju miwili ya penalti sambamba na kufunga penalti ya mwisho na kuitoa kimasomaso timu yake na kutinga fainali ya Kagame 2014 mjini Kigali Rwanda.


Timu za El merekh ya Sudani na APR ya Rwanda zimefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya m ichuano ya klabu bingwa Afrika mashariki na kati maarufu kama kagame baada ya kushinda michezo yao ya nusufainali hapo jana.
Wakati El merekh ikifunga KCCA ya Uganda kwenye nusu fainali ya kwanza iliyochezwa uwanja wa Amahoro mjini Kigali Rwanda kwa changamoto ya mikwaju  ya penalty 3 kwa 0, APR yenyewe nayo imetinga hatua hiyo kwakuifunga  ndugu zao Polisi Rwanga kwa mikwaju ya penalt 4 kwa 2.
APR na Polisi zilifikia hatua ya kupigiana matuta baada ya kutoka suluhu katika dakika 120 ndipo waliolazimika kupigiana changamoto ya mikwaju ya penalty wakati El merekh yenyewe pia iliiondosha KCCA ya Uganda kutokana na kufungana magoli 2 kwa 2 ndani ya dkk 120.
Kwamatokeo hayo hatua ya fainali itakayofanyika kesho mjini Kigali Rwanda   itakuwa baina ya El merekh ya Sudani na APR ya Rwanda pambano litakalochezwa kunako dimba la Amahoro.
Mbali na pambano hilo la fainali mchezo mwengine utakuwa ni wa kusaka mshindi wa tatu baina ya KCCA ya Uganda na Polisi ya Rwanda michezo yote ikichezwa kunako dimba la Amahoro.
                                           
                                 Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment