Baada ya
pazia la michuano ya Hepautwa cup 2014 kufunguliwa hapo jana katika uwanja wa kumbukumbu ya Samora mjini Iringa mashindano
hayo yanatarji kuendelea tena leo kwa mchezo mmoja.
Kwamujibu wa
ratiba hiyo timu ya Mlandege fc inataraji kuikabili Ilala fc kwenye uwanja huo
wa Samora hii ikiwa ni hatua ya awali ya mtoano ambapo timu inayoshinda ndiyo
inayosonga mbele na inayoshindwa inatoka.
Akizungumza katika
mchezo wa ufunguzi hapo jana mdhamini wa mashindano hayo Ndg.Nuru Hepautwa alisema
lengo la kuanzisha mashindano hayo ni kutoa fursa kwa vijana wa mjini Iringa na
mkoa wa Iringa kwaujumla kucheza soka.
Hepautwa aliwataka
wachezaji wote kucheza kwa nidhamu kwakuwa soka na ajira nzuri hivi sasa huku
akiahidi kutoa ushirikiano kuanzia
mwanzo hadi mwisho wa mashindano hayo.
Katika mchezo wa ufunguzi Makorongoni fc iliibuka na ushindi wa magoli 6 kwa 0 dhidi ya Gangilonga.
Katika mchezo wa ufunguzi Makorongoni fc iliibuka na ushindi wa magoli 6 kwa 0 dhidi ya Gangilonga.
Mdhamini wa mashindano ya Hepautwa cup 2014,Nuru Hepautwa akikagua timu hapo jana kwenye uwanja wa Samora.
Ifutayo ni ratiba ya michuano hiyo
hatua ya mtoano michezo yote ikichezwa katika uwanja wa kumbukumbu ya samora.
17/08/2014.
Mlandege 1 vs
0 Ilala fc.
18/08/2014.
Isakalilo 5 vs
4 ruaha.
19/08/2014.
Kitwiru vs
kihesa.
20/08/2014.
Mwangata vs
mtwivila city.
21/08/2014.
Kitanzini vs
mkwawa.
22/08/2014.
Mivinjeni vs
mshindo.
Timu ya
kwakilosa itaungana na timu zilizofuzu hatua ya mtoano kwamujibu wa kanuni za
mashindano hayo.
No comments:
Post a Comment