Mshambuliaji
wa klabu ya LA Galaxy ya nchini Marekani London Donovan ametangaza kustaafu
soka mara baada ya kumalizika kwa msimu mpya wa ligi kuu ya MLS (Major League
Soccer).
Akiwa na umri wa maiak 32 Donovan ameshafunga
magoli 57 kwenye michezo 156 kwenye timu
ya taifa ya Marekani na ndiye mfungaji wa muda wote wa timu hiyo.
Akizungumza na
waan dishi wa habari nchini Marekani Donovan amesema anajisikia furaha kucheza kwenye ligi kuu ya nchi hiyo nakuwashukuru wote waliomuunga mkono katika
kazi yake ya kucheza soka.
Pia nyota huyo amewahi kucheza michezo 22 na
kufunga magoli 2 akiwa kwa mkopo katika timu ya Everton ya nchini England mwaka 2010 na 2012 lakini pia amewahi
kuzichezea timu za Bayer Leverkusen na Bayern Munich.Aidha Donovani ambaye amecheza fainali za mwisho kwake za kombe la dunia mwaka 2010 nchini Afrika ya kusini ameahidi kuendelea kuwa karibu na watu mbalimbali waliyopo kwenye mchezo anaoupenda zaidi.
Donovan ambae hakuwepo kwenye kikosi cha marekani kilichoshiriki fainali za mwaka huu za kombe la dunia huko Brazil chini ya kocha mkuu Jurgen Klinsmann atahitimisha maisha yake ya soka mwezi wa 10 mwaka huu baada ya kumalizika kwa msimu wa ligi ya marekani MSL.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment