Pages

Ads 468x60px

Saturday, August 23, 2014

UCHAGUZI LIPULI FC SEPT 28 2014.

                             Mwenyekiti  wa kamati ya uchaguzi ya Lipuli fc Jackson Abraham Chaula.

 Uchaguzi wa kupata viongozi wapya wa timu ya soka ya Lipuli ya mkoani Iringa unataraji kufanyika tarehe 28 ya mwezi 9 mwaka huu ambapo nafasi mbalimbali zinawaniwa ikiwemo nafasi ya Uenyekiti ukatibu pamoja na wajumbe wa kamati ya utendaji.

Kwamujibu wa mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi huo Jackson Abraham Chaula  Amesema  muda wa kuchukua na kurudisha fomu za kugombea zitaanza kutolewa kesho tarehe 24/08/2014 kwa nafasi zote hadi tarehe 28 ya mwezi huu wa nane mwaka huu wa 2014.
Kwamujibu wa mwenyekiti wa kamati hiyo 29/08 hadi 30/08 mwaka huu kitafanyika kikao cha mchujo wa awali wa wagombea zoezi litakalosimamiwa na kamati hiyo ya uchaguzi.
31/08/2014  ni kuchapisha  na kubandika kwenye mbao za matangazo orodha ya awali ya wagombea  na tarehe 01 ya mwezi wa 9 ni kipindi cha kuweka pingamizi kwa wagombea zoezi litakalenda hadi 04/09/2014.
Tarehe 7/09 hadi 8/09 2014  kupitia pingamizi zote na kufanyia usaili wagombea wa uchaguzi huo na tarehe 7/09 hadi 8/09 2014 kipindi cha kupokea ,kusikiliza na kutoa majibu ya masuala ya kimaadili.
Pamoja na taratibu zingine zitakzofuata baada ya hapo kabla ya uchaguzi huo utakaofanyika September 28 mwaka huu sifa za muombaji  ni
1.Kuwa raia wa Tanzania.
2.Awe na sifa zinazohitajika kwa nafasi anayoiomba na awe amelipa ada ya uanachama kikamilifu tangu aanze uanachama.
3.Awe na kiwango cha chini cha elimu ya kuanzia kudato cha nne yenye uthibitisho kutoka baraza la mitihani la taifa.
4.Asiwe  aliyewahi kutiwa hatiani kwa kosa la jinai  kwa kutuhumiwa  kifungo.
5.Awe na umri angalau kuanzia miaka 25.
6.Awe ametimiza angalau miezi 6 ya uanachama.
7.Asiwe mwamuzi wa soka anayefanya shughuli za uamuzi kwa kipindi hiki.
Gharama za fomu.
Mwenyekiti ,makamu mwenyekiti,.Laki 1
Katibu na katibu msaidizi  …Laki 1.
Mweka hazina na mweka hazina msaidizi ...Elfu 50,
Wajumbe wa5 wa kamati  ya utendaji ..Elfu 50
Mwekahazina msaidizi……Elfu 50
Fomu zinapatikana VETA Iringa  onana na Ramadhani Mahano.
Mshindo kwa…..Fundi Rajabu.

                                          Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment