Pages

Ads 468x60px

Wednesday, August 13, 2014

MARTINO KOCHA MPYA WA TIMU YA TAIFA YA ARGENTINA.



                                     Gerardo Martino kocha mpya wa timu ya taifa ya Argentina.

Shirikisho la soka nchini Argentina limemtangaza kocha wa zamani wa Fc Barcelona Gerardo Martino kuwa kocha wa timu ya ya taifa kuchukua nafasi ya Alejandro Sabella aliyeachia ngazi mara baada ya kumalizika fainali za kombe la dunia ambapo Argentina ilifungwa goli 1 kwa 0 na Ujerumani.
Martino mwenye umri wa miaka 51 aliondoka Barcelona mwishoni mwa msimu uliopita  baada ya kuifundisha timu hiyo kwa mwaka mmoja  na kushindwa kutwaa taji hata mmoja kwa mara ya kwanza tangu msimu wa 2007-2008.
Martino alipewa kibarua cha kuifundisha Fc Barcelona  mwezi july mwaka 2013 kuchukua nafasi ya marehemu Tito Vilanova nakusaini mkataba wa miaka miwili lakini kutokana na kushindwa kupata mafanikio alifukuzwa kazi na nafasi yake ikachukuliwa na Luis Enrique.
Martino aliwahi kuwa kocha wa timu ya taifa ya Paraguay kati ya mwaka 2006 na 2011 na kuifikisha robo fainali katika fainali za kombe kla dunia mwaka 2010.
Martino anataraji kutambulisha kesho Alhamisi  mbele ya vyombo vya habari tayari kuwa kocha mkuu wa Argentina.

                                  Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment