Pages

Ads 468x60px

Sunday, August 10, 2014

HIKI NDICHO ALICHOONGEA NASRI JUU YA YEYE KUSTAAFU KUICHEZEA TIMU YA TAIFA.



                                            Samir Nasri.


Kiungo wa  klabu ya Manchester City  Samir Nasri amemshushia lawama nyingi kocha mkuu wa timu ya taifa ya Ufaransa Didier Deschamps na wachezaji wa timu ya taifa hilo kumfanya afikie uamuzi wa kustaafu kuitumikia timu hiyo.
 
Nasri amesema kuwa amekuwa akiwaza  kustaafu kuitumikia timu yake ya taifa tangu mwaka 2012 mara baada ya fainali za kombe la mataifa ya Ulaya  nasasa anathibitisha rasmi kustaafu kuitumikia timu ya taifa ya Ufaransa.
Nasri amesema hadhani kama atafikiria kubadili uamuzi wake maka timu ya taifa itaendelea kuwa chini ya kocha Didier Deschamps.
Nasri mwenye umri wa miaka 27 amesema amesikia taarifa kwenye vyombo vya habari kuwa baadhi ya wachezaji wa timu ya taifa walikuwa wanalalamika kwanini hakujumuishwa na kocha kwenye kikosi cha Ufaransa kilichokuwepo Brazil hali inayomaanisha hata wachezaji wenzake wapo katika makundi.

Nasri amesema kuwa kocha mkuu wa timu ya taifa alikaririwa na vyombo vya habari akisema hakumuita  katika timu ya taifa kutokana kumuona hana furaha  nakuongeza  kwamba ni mchezaji gani ambaye hufurahia kukaa benchi.

Nasri ambaye aliadhidiwa kutocheza michezo mitatu bada ya michuano ya Euro 2012 kutokana na kutoa lugha chafu kwa waandishi wa habari ameongeza kuwa familia yake haijisikii furaha na kitendo cha yeye kuanchwa kwenye kikosi cha taifa hivyo uamuzi wake wa kustaafu utawapunguzia maumivu.

Katika timu ya taifa Nasri amefunga magoli 5 katika michezo 41 aliyocheza.
                                 Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment