Super Mario Balotelli akiwa na baybe wake.
Wakati mshambuliaji Mario Balotelli
akitaraji kuwasili leo Uingereza kufanyiwa vipimo vya Afya mchana huu katika timu ya Liverpool hata akifaulu vipimo
hivyo hatopangwa kwenye mchezo wa
jumatatu ambapo Liverpool itakuwa
ikicheza na Manchester City.
Liverpool ambayo ipo tayari kumpatia
Balotelli mkataba wa miaka mitano na mshahara wa paundi laki moja na elfu
ishirini kwa juma imebainisha kuwa watahitaji kutambua utayari wa mchezaji huyo
pamoja na suala la nidhamu kabla ya kupangwa kuchezwa.
Tayari Liverpool imeshakubaliana na
AC Milan juu ya kuuziana mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 aliyewahi kuichezea
Manchester City kwa uhamisho wa paundi milioni 16 na wengi wanadhani kuwa
endapo Balotelli atafaulu vipimo ataikabili timu yake ya zamani ya Manchester
City.
Samwel Eto'o.
Katika hatua nyingine Uongozi wa
Liverpool upo tayari kumpa makataba wa mwaka mmoja mchezaji Samweli Eto’o ambaye
amemaliza mkataba wake na Chelsea msimu uliopita ili kuiongezea nguvu safu yake
ya ushambuliaji.
Mkuleblogsport.com.
Super Mario.......!
ReplyDeleteUsajili wa kweli ila ndo ngumi mkononi......njoo utupe raha, Mario Balotelli mzee wa magazeti haishiwi vituko.
Mwana wa Madunda