Diego Semione aliyevaa suti hapo akimzungumza na kamisaa wa mchezo kwenye pambano dhidi ya Real madrid juma lililopita.
Uongozi wa
mabingwa wa ligi kuu ya Hispania klabu ya Atletico Madrid umesema
haujakubaliana na adhabu aliyopewa kocha wao mkuu Diego Semione ya kufungiwa michezo 8 iliyotolewa na
shirikisho la soka nchini humo baada ya kuonyesha utovu wa nidhamu kwenye
mchezo wa Spanish Super cup.
Rais wa
klabu hiyo Enrique Cerezo amesistiza kwamba hawakubaliani na adhabu hiyo ambayo
imetokana na kocha huyo kuvunja sheria uwanjani siku ya mchezo dhidi ya Real
Madrid juma lilopita kwenye uwanja wa
Vicente Calderon.
Rais huyo
amesema mara baada ya kuwasilisha rufaani yao ya kupinga adhabu hiyo watasubiri majibu lakini akisistiza adhabu hiyo ni kubwa kulikokosa alilolifanya kocha huyo raia wa
Argentina.
Katika
mchezo huo uliochezwa mwishoni mwa juma lilopita kocha huyo alikiuka sheria
kwakuvuka eneo analotakiwa kukaa na pia alimsukuma kamisaa wa pambano hilo akishinikiza
mchezaji wake aliyekuwa anatibiwa nje ya uwanja aruhusiwe kurudi uwanjani
haraka.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment