Mustakabali wa rufaani ya
mshabuliaji mpya wa Fc Barcelona Luis
Suarez unataraji kujulikana leo ambapo mahakama ya masuala soka duniani CAS mjini Uswis inasikiliza na
kufanya maamuzi juu ya adhabu ya kufungiwa kwa mchezaji huyo miezi minne.
Suarez ambaye amepigwa marufuku
kuingia kwenye uwanja wowote wa soka
hata wa timu yake ya Fc Barcelona sambamba na kutofanya mazoezi ya pamoja na
wachezaji wenzake wa kikosi hicho aliwasilisha
rufani hiyo kupinga adhabu aliyopewa na shirikisho la soka duniani Fifa.
Katika mahakama hiyo ya CAS iliyopo
mjini Lausanne Uswis Suarez atawakilishwa na wanasheria wake akiwemo Daniel Cravo na mara baada ya rufani
hiyo kusikilizwa taarifa rasmi itatolewa kwa vyombo vya habari.
Suarez kwasasa anatumikia adhabu ya
kutocheza soka kwa miezi minne sambamba na kutoitumikia timu yake ya taifa ya
Uruguay michezo minane kutokana na kumng’ata nyota wa Italia Giorgio Chiellini
kwenye fainali za kombe la dunia mwaka huu zilizomalizika mwezi ulipita nchini
Brazil.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment