Kiungo wa mabingwa wa ligi kuu ya Ujerumani Bayern
Munich Javi Martinez leo
anataraji kufanyiwa upasuaji wa goti baada ya kumia kwenye pambano la jana
baina ya timu yake na Borrusia Dortmund kuwania kombe la DFL Super Cup ambapo
kikosi chake kilifungwa magoli 2 kwa 0.
Javi Martinez akipata msaada kutoka kwa madaktari wa Fc Bayern Munich.
Javi Martinez ambaye ni
mchezaji wa zamani wa Atletico Bilbao imethibitika kuwa atakaa nje kwa muda miezi minne kupatiwa matibabu ya jeraha
la goli alilolipata kwenye mchezo huo wa jana.
Katika
mchezo huo magoli ya Borussia Dortmund chini ya kocha Jurgen Klopp yalifungwa
na wachezaji Henrikh Mkhitaryan dakika ya 23 pamoja na Pierre-Emerick Aubameyang dakika 62
na kuiwezesha timu yao kushinda taji hilo.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment