Wednesday, August 27, 2014
CRYSTAL PALACE YAMTANGAZA WARNOCK KUWA KOCHA MPYA.
Neil Warnock kocha mpya wa Crystal Palace.
Klabu ya soka ya Crystal Palace imemtangaza Neil Warnock kuwa kocha wao mpya kwa mkataba wa miaka miwili kuchukua nafasi ya Tony Pulis aliyeachia ngazi juma lililopita.
Warnock mwenye umri wa miaka 65 aliwahi kuifundisha Palace kati ya mwaka 2007 na 2010 na sasa atakuwa akisaidiana na kocha msaidizi Keith Millen ambaye alipewa jukumu la kocha mkuu wa muda baada ya Tony Pulis kuachia ngazi.
Kocha huyo mpya ameahidiwa na uongozi wa Palace kuwa atapewa fungu la kufanya usajili kabla ya dirisha kufungwa jumatatu ijayo.
Ikiwa chini ya kocha msaidizi Keith Millen tangu kuanza kwa msimu huu wa ligi kuu ya England Crystal Palace ilipoteza mchezo wa kwanza dhidi ya Arsenal kwakufungwa magoli 2 kwa 1 ikiwa ugenini kabla ya kufungwa magoli 3 kwa 1 na West ham huku ikishinda goli 3 kwa 0 dhidi ya Walsall kwenye mzunguko wa pili wa Capital one Cup.
Mkule.blogsport.com
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment