Mwamuzi maarufu barani Ulaya raia wa
Uingereza Howard Webb amestaafu kazi hiyo na kuwa mkurugenzi mkuu wa michezo ya
kimataifa .
Webb mwenye umri wa miaka 43 alianza
kazi ya uamuzi wa soka tangu mwaka 1989
nakutambulishwa rasmi katika ligi kuu ya England mwaka 1998 kabla ya kusimamia michezo mbalimbali ya
klabu bingwa Ulaya na kombe la dunia.
Webb ambaye ni askari mstaafu wa Uingereza mchezo wake wa kwanza akiwa mwamuzi wa ligi kuu ya England ulikuwa mwezi wa 10 mwaka 2003 kabla ya kujumuishwa kwenye orodha ya waamuzi wa shirikisho la soka dunia Fifa miaka miwili baadae.
Mwamuzi huyo mkongwe majukumu yake yatakuwa ni pamoja na kuwa
mkufunzi wa waamuzi na masuala mbalimbali ikiwa na kufundisha mambo mbalimbali
kwenye jamii yanayohusu uamuzi wa soka.
Akizungumza mara kustaafu Webb
amesema anajisikia furaha kuanza ukurasa mpya wa maisha yake baada ya taaluma
yake ya uamuzi wa soka kwa miaka 25 nakuongeza kuwa amejifunza mengi
kwenye fani hiyo.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment