Nyota mpya wa timu ya Real Madrid raia wa Colombia Jemes Rodriguez amesema anamatumaini makubwa ya kufunga magoli kadri atakavyopata nafasi katika msimu wake wa kwanza akiwa na klabu hiyo ya Hispania.
Jemes ambaye alifunga goli lake
la kwanza akiwa na Real usiku wa kuamkia
leo kwenye mchezo wa Spanish Super cup dhidi ya Atletico Madrid uliomalizika kwa
sare ya goli 1 kwa 1 ameeleza kuwa na furaha
baada ya kufungua ukurasa wake wa kwanza wa magoli akiwa timu hiyo.
Nyota huyo ambaye amesajiliwa
kutoka Monaco ya Ufaransa baada ya kuonyesha kiwango kikubwa kwenye fainali za
kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil amebainisha kuwa anaimani kuwa Cristiano
Ronaldo atarejea kiwango chake baada ya kuzongwa na majeruhi.
Katika mchezo huyo wa kuashiria
kuanza kwa ligi kuu ya Hispania itakayoanza
jumamosi ya wiki hii Rodriguez alichukua nafasi ya Ronaldo ambaye
alipumzishwa na kocha Carlo Ancelotti amesema mreno huyo anataraji
kufaniwa uchunguzi.
Rodriguez akijaribu kumiliki mpya kwenye mbano la usiku wa kuamkia leo dhidi ya Atletico madrid.
Nyota wa Real madrid Gareth Bale akijaribu kuwatoka wachezaji wa Atletico Madrid kwenye pambano la Spanish Super cup lililomalizika kwa sare ya goli 1 kwa 1.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment