Shirikisho
la soka nchini Italia maarufu kama FIGC
limemtangaza kocha wa zamani wa klabu ya Juventus Antonio Conte kuwa vkocha mpya wa timu ya taifa ya nchi hiyo .
Conte mwenye umri wa miaka 45 amechaguliwa na shirikisho hilo kurithi mikoba ya Cesare Prandelli aliyejiuzulu baada ya kuondoshwa mapema katika michuano ya kombe la dunia iliyomalizika mwezi julai nchini Brazil.
Shirikisho la soka nchini Italia limethibitisha taarifa hiyo katika tovuti yake kuwa tayari Conte amesaini mkataba wa miaka miwili ya kukinoa kikosi hicho hadi mwaka 2016.
Kuchaguliwa kwa kocha Conte imekuja siku chache baada ya nchi ya Italia kumchagua Raisi mpya wa shirikisho hilo Carlo Tavecchio kurithi mikoba ya Giancarlo Abete alijiuzulu kutokana na nchi yake kushindwa kutwaa kombe la dunia msimu huu.
Mkule.blogsport.com
Conte mwenye umri wa miaka 45 amechaguliwa na shirikisho hilo kurithi mikoba ya Cesare Prandelli aliyejiuzulu baada ya kuondoshwa mapema katika michuano ya kombe la dunia iliyomalizika mwezi julai nchini Brazil.
Shirikisho la soka nchini Italia limethibitisha taarifa hiyo katika tovuti yake kuwa tayari Conte amesaini mkataba wa miaka miwili ya kukinoa kikosi hicho hadi mwaka 2016.
Kuchaguliwa kwa kocha Conte imekuja siku chache baada ya nchi ya Italia kumchagua Raisi mpya wa shirikisho hilo Carlo Tavecchio kurithi mikoba ya Giancarlo Abete alijiuzulu kutokana na nchi yake kushindwa kutwaa kombe la dunia msimu huu.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment