Kocha mkuu wa machampion wa klabu bingwa
Ulaya Real Madrid Carlo Ancelotti amezionya timu za Arsenal na Chelsea
zinazomnyemelea kiungo wake Sami Khedira
kwakusema nyota huyo raia wa Ujerumani hauzwi.
Khedira ambaye amekuwa akitajwa kuwindwa
na vilabu vilivyotajwa,kocha Carlo Ancelotti amesema mchezaji huyo hatoondoka
Santiago Bernabeu ataendelea kuwa mali ya Real Madrid hadi mkataba wake
utakapomalizika mwezi wa sita 2015.
Akizungumza kuelekea katika mchezo wa
Uefa Super Cup kocha huyo amesema Khedira ni mchezaji aliyopo kwenye mipango
yake na hawatakuwa tayari kumuuza kwa sasa.
Katika hatua nyingine nyota wa timu hiyo
Gareth Bale amesema amejipanga msimu huu watwae mataji yakutosha kwakuwa kikosi
chao hivi sasa kimeimariha hivyo kinakila sababu ya kushinda makombe mengi
zaidi ya msimu uliopita.
Mkule.blogsport.com
No comments:
Post a Comment