Pages

Ads 468x60px

Saturday, August 9, 2014

ZIJUE AHADI NA MIPANGO YA MGOMBEA WA UKATIBU MKUU WA CHAMA CHA SOKA MKOA WA IRINGA DOCT.ALLY NGARA.




           Doct.Ally Ngara,mgombea wa nafasi ya ukatibu mkuu wa (IRFA)unaotaraji kufanyika 23.08.2014.

Wakati kampeeni zikiendelea kwenye uchaguzi wa chama cha soka mkoani Iringa (IRFA)mgombea wa nafasi ya ukatibu mkuu Doct.Ally Ngara amesema endapo akifanikiwa kushinda kwenye uchaguzi huo ataleta mapinduzi ya soka  katika mkoa huo.
Ngara ambaye anakabiliwa na upinzani kutoka kwa mgombe mwenzake Ramadhani Mahano amesema mara baada ya kuchaguliwa  atafanya mambo mhimu ambayo yatakuwa dira nzuri ya kuliendelezaoka la mkoa huo ambalo limepoteza mwelekeo kwa kiasi kikubwa kwa hadi sasa ni zaidi ya miaka 10 mkoa huo hauna timu ya ligi kuu baada ya Lipuli kushuka daraja miaka 13 iliyopita.
1.Kuhakikisha anarejesha mshikamano miongoni mwa viongozi wa vyama vya soka katika vilaya za mkoa huo na ule wa mkoa (IRFA)pamojana na wadau wa mchezo huo.
2.Kuvunja matabaka ambayo yapo  kwakuwa uwepo wa matabaka  utasababisha mpasuko ambao utafanya  soka lisiiende kama ambavyo wadau wengi wanahitaji.
3.Uongozi wake hautafumbia macho masuala ya upangaji wa matokeo kwa vilabu vya soka mkoani humo kuanzia ngazi ya chini hadi juu na kiongozi yeyote wa klabu au mchezaji atakaebainika kufanya tabia hiyo atachukuliwa hatua kali za kinidhamu.
4.Kuhakikisha chama cha soka kinakuwa na ofisi yake ambayo itashughulikia masuala ya mpira pekee na itakuwazi kwa wanamichezo hususani mpira wa miguu kutoa mawazo yao,malalamiko yao ambayo wanayo  jambo litakalo saidia uongozi wake kuwa na utendaji bora zaidi.
(Hadi sasa uongozi wa chama cha soka hauna ofisi maalumu kwani hata katibu aliyepita alikuwa anatumia ofisi yake binafsi)
5.Kutii kiu ya wadau wa mpira wa miguu mkoani Iringa ambao wanamapenzi makubwa na mchezo huo na sasa wanahitaji walau kuona ligi kuu ikichezwa kwenye mkoa huo.Amesema mara baada ya kuchaguliwa atahakkikisha anapandisha timu zote zilizopo ligi daraja la kwanza Lipuli fc na Kurugenzi fc ya Mafinga kwenda ligi kuu na kama sio zote basi hata mmoja na hilo litafanyika katika msimu wa kwanza atakaokuwa madarakani.Atahakikisha hilo linafanikiwa kwakushirikiana na viongozi waliopo na wadau wote wenye kiu ya kuona ligi kuu.
6.Kuwaheshimu na kuwathamini wale wote watakaotoa mali zao mawazo yao ya  kuendeleza mpira wa miguu kwenye mkoa wa Iringa kwakuwa kufanya hivyo hakutajenga hofu tena iliyopo kwa miongoni mwao ambao wameshapoteza imani na soka la mkoa huo.
7.Kuwashirikisha wakongwe wote waliowahi kucheza soka katika mkoa wa Iringa na wale wanaoijua vyema historia ya soka la mkoa huo kwakuwa wao ndio wanaojua jinsi mchezaji anavyoumia anapokuwa uwanjani.
Amesema atahakikisha Wakongwe hao wanaheshiwa na kuthaminiwa huku wakishirikishwa katika mikutano mbalimbali ya maendeleo ya soka la mkoa wa Iringa jambo ambalo halifanyiki sasa na badala yake wanachukuliwa kama watu wa kawaida.
8.Kuanzisha ligi mbalimbali nyingi zenye masharti nafuu ili kutoa nafasi ya vijana kucheza mpira.Amesema wapo wadau mbalimbali ambao wamekuwa mstari wa mbele kuanzisha ligi au mashindano mbalimbali ili kusaidia maendeleo ya soka la mkoa huo kwenda mbele.
9.Kusimamia soka la wanawake na viongozi wa chama cha soka la wanawake waliopo  mkoani humo na atahakikisha kunakuwa na ligi mbalimbali za soka la wanawake katika wilaya za mkoa huo.Amesema hilo litasaidia kukua kwa maendeleo ya soka la wanawake mkoa wa Iringa.
10.Uhusiano kuwa mzuri baina ya chama cha soka mkoani humo na vyama shiriki kama chama cha waamuzi,chama cha madaktari,chama cha makocha,na vyama vingine vyote shiriki ili pale cha chochote shiriki kinapokuwa na matatizo washirikiane kwa pamoja kutatua changamoto zinazowakabili.
Amesema suala la kupata kocha yeyote wa timu ya mkoa iwe ya vijana au wakubwa mchakato huo utashirikisha chama cha makocha mkoa ili kusikiliza mawazo yao na kuona kocha yupi anayefaa.
Ngara amesema kero zote za waamuzi zitashughulikiwa ili kurejesha heshima kwa waamuzi wa soka inayoonekana kuporomoka kwa kiasi kikubwa na pia kuhaklikisha taaluma ya urefarii wa soka inaanzia katika ngazi ya watoto wadogo.

                                 Mkule.blogsport.com.

No comments:

Post a Comment