Mabingwa mara
20 wa ligi kuu ya England Manchester United imeweka hadharani wachezaji wake
inayowauza hivi sasa na kocha mkuu wa mashetani hao wekundu Lous Van Gaal
ameitaka klabu yeyote inayowahitaji kuwasiliana na uongozi wa timu hiyo.
Majina ya
nyota wanaouzwa yametangazwa siku 7 kabla ya kuanza kwa ligi kuu ya nchini
England na ni sehemu ya tamko alilolitoa kocha Louis Van Gaal baada ya kurejea England
wakitokea Marekan ambapo timu hiyo ilikuwa ikicheza michezo mbalimbali ya kirafiki
na kufanya vyema kwa asilimia kubwa.
Van Gaal
alitangaza kuwa baada ya kuwapa wachezaji wote 26 kucheza katika mechi za
majaribio ameshajua uwezo wa mchezaji mmoja mmoja hivyo kumpa nafasi ya kuona
ni nyota wapi hawatakuwa kwenye mipango yake.
Wafuatao kwenye
picha ni wachezaji wanaouzwa na thamani zao.
Pamoja na
hayo kocha huyo anatarjiwa kumtangaza nahodha mpya wakati wowote baada ya
aliyekuwa akishikilia kitambaa cha unahodha Nemanja Vidic kuhamia Inter Milan
ya Italia.
Wanaopendekezwa
kuwa huenda mmoja wao akawa nahodha ni Robin Van Persie na Wayne Rooney.
Mkule.blogsport.com.
No comments:
Post a Comment