Pages

Ads 468x60px

Monday, August 25, 2014

KUFUATIA KIFO CHA MCHEZAJI,SHIRIKISHO LA SOKA NCHINI ALGERIA LASIMAMISHA MICHEZO YA LIGI MWISHONI MWA JUMA HILI.



                        Marehemu  Albert Ebosse  enzi za uhai wake.

Shirikishoa la soka nchini Algeria  FAF limesimamisha michezo yote ya ligi daraja la kwanza  iliyokuwa ichezwe mwishoni mwa juma hili kufuatia kifo cha mchezaji Albert Ebosse kilichotokea jana  kwakupigwa na kitu kigumu akiwa uwanjani.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 alifariki mwishoni mwa mchezo baina ya timu yake ya JS Kabylie  na USM Alger  uliomalizika kwa JS Kabylie kufungwa magoli 2 kwa1  huku goli pekee la timu hiyo likiwa limefungwa na marehemu Albert Ebosse's.
Taarifa ya shirikisho hilo imesema kuwa michezo yote iliyokuwa ichezwe tarehe 29 na 30 ya mwezi huu haitokuwepo hadi itakapotangazwa  hapo baadae mara pindi uchunguzi wa tukio hilo kukamilika na hatua zaidi kuchukuliwa.
Tayari raisi wa shirikisho la soka barani Afrika Caf Issa Hayatou amewapigia simu viongozi wa shirikisho la soka nchini Algeria  akiwataka kuchukua hatua kali kwa ukatili huo uliofanywa na mashabiki wahuni na  CAF haitokuwa tayari kuvumilia uovu huo viwanjani.


                                         Marehemu  Albert Ebosse  enzi za uhai wake.
                                      
                                     Mkule.blogsport.com

No comments:

Post a Comment